JIACHIE: MKURUGENZI WA MASHTAKA AFUNGUA MAFUNZO YA UELIMISHAJI KUHUSU MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI


NA SEBERA FUGENCE – AFISA UHUSIANO MWANDAMIZI (WCF), MOROGORO

IMEELEZWA kuwa waajiri ambao hawajisajii na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Mashtaka Mhe. Biswalo Mganga katika mafunzo ya uelemishaji wa Mawakili wa Serikali wa Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Morogoro, Lindi na Mtwara yaliyofanyika Mkoani Morogoro jana. (leo)

Mheshimiwa Mganga alisema   hatua za kisheria zitachukuliwa kwa waajiri watakaobainika kutenda makosa mengine yakiwemo ya kutowasilisha michango katika Mfuko kwa wakati.

Alisema lengo la Serikali ni kuona kila mfanyakazi anayeumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi anapata mafao yake kama ambavyo imeeekezwa katika Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi  Sura 263 ikisomwa pamoja na kanuni zake za mwaka 2016.

“Mafunzo haya yatatoa fursa kwa Ofisi yangu na Maafisa wengine kueleza uzoefu wao kuhusu  namna ya kuendesha Mashauri ya Jinai zikiwemo changamoto wanazokutana nazo na mapendekezo ya utatuzi wa changamoto hizo hasa pale wanaposhughulikia kesi dhidi ya waajiri wanaokiuka sheria.
Alisema Ofisi yake ni mdau muhimu sana katika kuhakikisha kuwa matakwa ya Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi yanatekelezwa kikamilifu na wale wanaoshindwa kutekeleza wajibu wao wanachukuliwa hatua stahiki za kisheria.

Nae Mkurugenzi  Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) nchini  Bw. Masha Mshomba alisema  Ofisi  ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali  ipo kwa mujibu wa Sheria ya Ibara ya 59B ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 na moja kati majukumu yake ya msingi ni kufungua, kusimamia  na kuendesha mashauri ya jinai katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Alisema Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali ni mdau muhimu sana katika kuhakikisha malengo ya Mfuko huo yanafikiwa kwani ndio wasimamizi wakuu katika uendeshaji mashauri ya jinai yakiwemo makosa ya jinai yaliyoainishwa kwenye Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi.
Aliitaja changomoto inayoikabii Mfuko huo kuwa ni  idadi kubwa ya waajiri ambao hawajajisajili na hawachangii kwenye Mfuko na kuongeza kuwa changamoto hiyo isipopatiwa suluhisho la haraka itaathiri uwezo wa  Mfuko kulipa fidia kwa wafanyakazi.

Alisema hadi kufikia juni 30, 2017 Mfuko umelipa fidia ya kiasi cha Shilingi 613,843,555.64 ikiwa ni gharama za matibabu fidia ya ulemavu wa muda mfupi na ulemavu wa kudumu.Kwa upande wa usajili Bw. Mshomba amesema hadi kufikia juni 30, 2017 mfuko tayari ulikuwa umesajii waajiri 7,857 ambapo hadi kufikia juni 31, 2017 inakadiriwa kuwa  zaidi ya waajiri 13,918 waliopo Tanzania Bara hawajasajiiwa kwenye Mfuko.

Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ni Taasisi ya Hifadhi ya Jamii iiyoanzishwa chini ya kifungu cha 5 cha Sheria ya Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi Sura 263 marejeo ya mwaka 2015 kwa lengo la kushughuikia masuala ya fidia kwa wafanyakazi wanaoumia ama kuugua ama kufariki wakati wakitekeeza majukumu ya mwajiri kwa mujibu wa mikataba ya ajira zao.

Mkurugenzi  Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) Bw. Masha Mshomba akimkaribisha mgeni rasmi ambaye ni Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Bw. Biswalo Mganga kwenye Mafunzo ya Uelimishaji kuhusu Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF)  kwa Mawakii wa Serikali wa Mikoa ya Dar es Saaam, Morogoro, Lindi na Mtwara yaliyofayika mkoani Marogoro leo Oktoba 4, 2017.

Baadhi ya Washiriki wa Mafunzo wakimsikiliza Mkurugenzi wa Mashtaka katika Mafunzo ya Uelimishaji kuhusu Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF)  kwa Mawakii wa Serikali wa Mikoa ya Dar es Saaam, Morogoro, Lindi na Mtwara yaliyofayika mkoani Marogoro
Mkurugenzi wa Bw. Mashtaka Biswalo Mganga akifungua Mafunzo ya Uelimishaji kuhusu Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF)  kwa Mawakii wa Serikali wa Mikoa ya Dar es Saaam, Morogoro, Lindi na Mtwara yaliyofayika mkoani Marogoro
Mkurugenzi wa Mashtaka Biswalo Mganga (wa nne kutoka kushoto akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo ya Uelimishaji kuhusu Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF)  kwa Mawakii wa Serikali wa Mikoa ya Dar es Saaam, Morogoro, Lindi na Mtwara yaliyofayika mkoani Marogoro

READ MORE



from Habari Za Tanzania
vRead More

Comments

Popular This Week

IGP SIRRO:NCHI YETU IKO SALAMA, NA TUNAO UWEZO WA KUFANYA UCHUNGUZI | Darmpya

MBUNGE SINGIDA MAGHARIBI ELIBARIKI KINGU (CCM) AWEKA HISTORIA | Darmpya

TAWLA YATOA MAFUNZO YA JINSI YA KUSHUGHULIKIA WATOTO WALIO KATIKA UKINZANI NA SHERIA | VIJIMAMBO

Wasanii watakaokiwasha Tigo Fiesta jijini Mwanza watembelea Duka la Tigo leo. | Mrisho’s Photography

“Ukipata mshtuko wa moyo, usipopata huduma ndani ya dk 90 ni kifo” – JKCI | Millardayo

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

MSUVA AWA MTAMU APIGA MBILI PEKE YAKE, DIFAA EL JADIDA | Darmpya

Popular This Month

IGP SIRRO:NCHI YETU IKO SALAMA, NA TUNAO UWEZO WA KUFANYA UCHUNGUZI | Darmpya

TAWLA YATOA MAFUNZO YA JINSI YA KUSHUGHULIKIA WATOTO WALIO KATIKA UKINZANI NA SHERIA | VIJIMAMBO

MBUNGE SINGIDA MAGHARIBI ELIBARIKI KINGU (CCM) AWEKA HISTORIA | Darmpya

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

Wasanii watakaokiwasha Tigo Fiesta jijini Mwanza watembelea Duka la Tigo leo. | Mrisho’s Photography

“Ukipata mshtuko wa moyo, usipopata huduma ndani ya dk 90 ni kifo” – JKCI | Millardayo

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

Majeshi ya Iraq yapiga hatua kuishambulia IS

Popular All Time

MPOGOLO AWATAKA VIONGOZI MKOANI DODOMA KUSHUKA CHINI KUIMARISHA MASHINA…WAKULIMA WA ZABIBU WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI. | Darmpya

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

MSUVA AWA MTAMU APIGA MBILI PEKE YAKE, DIFAA EL JADIDA | Darmpya

MABONDIA WAWILI WA TANZANIA WACHEZEA KICHAPO USIKU MMOJA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

“SIJAONA SIMBA YA KUIFUNGA AZAM KESHO” – NGAONA | Darmpya

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

BABA NA MWANAE NA SHEMEJI MTU WAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA | Darmpya

MAFUNDI UMEME WATAKIWA KUWA NA LESENI YA EWURA KUPUNGUZA ‘VISHOKA’ NJOMBE | Darmpya