DEREVA WA TUNDU LISSU ANA MAJIBU KWA JESHI LA POLISI




Jeshi la Polisi nchini limesema bado linamhitaji dereva wa Mbunge wa singida Mashariki, Tundu Lissu, ili aweze kutoa majibu ya maswali mengi juu ya tukio la mbunge huyo kupigwa risasi mjini Dodoma Septemba 7, mwaka huu.

Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) Simon Sirro amesema hayo leo Jumatano mkoani Mtwara, wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuongeza kuwa upelelezi wa tukio hilo bado unaendelea ili kukamilisha uchunguzi.

“Chadema (Chama cha Demokrasia na Maendeleo), wanasema yule dereva anapatiwa matibabu ya kisaikolojia nchini Kenya, wakati kila siku kwenye mitandao tunaona picha zake anawaka tu hii inatupa wasiwasi kwa kuwa majibu ya maswali mengi tuliyo nayo anayo yeye, kwa sababu haiwezekani aendelee kupiga picha na kung’aa vile lakini wanasema ameathirika kisaikolojia, ” amesema IGP Sirro.

Hivi karibuni, Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, alisema dereva huyo yuko nchini Kenya anapatiwa matibabu ya kisaikolojia baada ya kushuhudia tukio hilo la Lissu kushambuliwa kwa risasi wakiwa pamoja kwenye gari. 

Lissu bado anatibiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya baada ya shambulio hilo.

READ MORE



from Habari Za Tanzania
vRead More

Comments

Popular This Week

HISTORIA YA WANGONI NA LILIPOTOKA JINA LA SONGEA | noreply@blogger.com (Lewis Mbonde)

MKEMIA MKUU: ‘Wanafunzi wanaoenda vyuoni wapimwe matumizi ya dawa za kulevya’ | Millardayo

Sina Beef Na Mange Kimambi Ananipenda Na Ananikubali : Wolper – Jicho La Uswazi | Mcinika Wa Lamar

KESI YA KUPINGA KUONDOLEWA CHANEL ZA NDANI KWENYE VISIMBUZI KUTAJWA OCTOBA 18 | Darmpya

MAMILIONI YA MFUKO WA JIMBO NYAMAGANA YAMWAGWA SOKO LA MLANGO MMOJA. | Darmpya

Kesi ya Aveva, Kaburu TAKUKURU yakiri upelelezi haujakamilika | Millardayo

Popular This Month

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA BILL GATES NA KAIMU BALOZI WA MAREKANI NCHINI | MICHUZI BLOG

HISTORIA YA WANGONI NA LILIPOTOKA JINA LA SONGEA | noreply@blogger.com (Lewis Mbonde)

Dubai yazindua jengo refu zaidi duniani lenye ghorofa 75 | Darmpya

Birdman wa CashMoney anakuja Tanzania | Millardayo

Popular All Time

MPOGOLO AWATAKA VIONGOZI MKOANI DODOMA KUSHUKA CHINI KUIMARISHA MASHINA…WAKULIMA WA ZABIBU WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI. | Darmpya

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

MSUVA AWA MTAMU APIGA MBILI PEKE YAKE, DIFAA EL JADIDA | Darmpya

MABONDIA WAWILI WA TANZANIA WACHEZEA KICHAPO USIKU MMOJA | Darmpya

“SIJAONA SIMBA YA KUIFUNGA AZAM KESHO” – NGAONA | Darmpya

MAFUNDI UMEME WATAKIWA KUWA NA LESENI YA EWURA KUPUNGUZA ‘VISHOKA’ NJOMBE | Darmpya

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

BABA NA MWANAE NA SHEMEJI MTU WAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA | Darmpya