Panya Road wa Mbagala watiwa mbaroni
Dar es Salaam. Jeshi la polisi mkoa wa Temeke limewakamata watu zaidi ya 15 wanaodaiwa kuwa ni Panya Road waliovamia na kuwapora watu waliokuwa wakitoka kwenye tamasha la kuinua vipaji lililoandaliwa na redio ya Clouds.
Wahalifu hao wanadaiwa kufanya uhalifu rmaeneo ya Sabasaba, Temeke, huku wakiwa na silaha za kijadi ikiwamo mapanga maeneo ya Sabasaba.
Kamanda wa polisi mkoa huo,Gilles Muroto alisema Oktoba 15 saa 11 jioni liliandaliwa tamasha la kuinua vipaji na Clous FM ambapo vijana hao walishiriki na baadaye kufanya uhalifu huo.
Alisema baada ya tamasha hilo kwisha watuhumiwa hao wanaodaiwa kuwa zaidi ya 50 waliingia mtaani huku na kuelekea eneo la sabasaba wakiwa na mapanga,visu,bisibisi kwa ajili ya kufanyia uhalifu.
Muroto alisema wakati wakielekea eneo hilo ndipo wananchi waliwadhibiti na kuwakamata vijana sita kati ya hao mmoja alifariki wakati akipelekwa hospitali,wawili wamelazwa katika hospitali ya rufaa ya temeke na watatu walitoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ambapo walikamatwa watuhumiwa hao.
"Hawa watuhumiwa watatu walitoa ushirikiano na waliwataja wenzao jumla ya vijana 16 walikamatwa ukimuondoa yule aliyefariki,"alisema Muroto.
Comments