SEDUCE ME ILIVYONOGA NA BAISKELI ZA ROSTAM FIESTA MWANZA – Bingwa | Bingwa


 

NA MWANDISHI WETU

WIMBO wa Seduce Me wa mkali wa Bongo Fleva, Ali Kiba, ameendelea kubamba katika maeneo mbalimbali, wikiendi iliyopita ukiwachizisha vilivyo wakazi wa Mwanza waliohudhuria tamasha la Tigo Fiesta 2017, kwenye Uwanja wa CCM Kirumba.

Lakini pia, uhondo wa wimbo huo ulinogeshwa zaidi na wakali wa hip hop, Roma Mkatoliki na Stamina, wanaounda umoja walioupa jina la Rostam, ambao walipanda jukwaani kivingine kwa kila mmoja kuwa na baiskeli yake na kuweka kitu tofauti kwenye wimbo wao wa Huku Ama Kule.

 

Manjonjo hayo yaliyofanywa na Rostam pamoja na uhondo wa Seduce Me, uliufanya Uwanja wa CCM Kirumba kulipuka kwa shangwe kutoka kwa mashabiki wa burudani waliofika uwanjani hapo kupata burudani kutoka kwa sanii wao wakali wa hapa nchini.

 

Kampuni ya Simu za mkononi ya Tigo Tanzania, alikuwa ni msanii wa kufokafoka, Rosa Ree, ambaye alifungua pazia la burudani na kuonyesha jinsi gani anakuja kwa kasi katika muziki pale alipoimba kwa umahiri wa hali ya juu nyimbo zake, zikiwamo Mchaga Mchaga na Up In The Air.

 

Baada ya msanii huyo, alifuatia mwanadada Lulu Diva, ambaye naye alikonga nyoyo za mashabiki kama ilivyokuwa kwa sanii wengi waliopata nafasi ya kufanya yao siku hiyo, Ommy Dimpoz, Rayvanny, Fid Q, Joh Makini, Ben Pol, Nandy, Jux, Maua, Weusi, Aslay, Young Killer, Darasa, Bill Nas, Future JNL, Bright, Eduboy na wengineo.

Kwa ujumla, tamasha hilo lilifana vilivyo jijini Mwanza, ambapo mashabiki lukuki walihudhuria kuonyesha jinsi Watanzania wanavyopenda burudani, lakini pia wasanii wao.

Akizungumzia tamasha hilo, Meneja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Edgar Mapande, alisema mwaka huu wameamua kudhamini ili kusaidia vipaji vya wasanii na kuwaletea wateja wao burudani, kadhalika kuwapatia vifurushi mara wanunuapo tiketi za Tigo Fiesta kwa Tigopesa.

“Mteja wetu akinunua tiketi kwa Tigopesa, anapata Mbs 100, dakika 100 na sms 100 bure,” alisema Mapande na kuongeza kuwa, tamasha hilo litaendelea Ijumaa hii mkoani Tabora kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi.

The post SEDUCE ME ILIVYONOGA NA BAISKELI ZA ROSTAM FIESTA MWANZA appeared first on Bingwa.

READ MORE



from Habari Za Tanzania
via Read More

Comments

Popular This Week

HISTORIA YA WANGONI NA LILIPOTOKA JINA LA SONGEA | noreply@blogger.com (Lewis Mbonde)

MKEMIA MKUU: ‘Wanafunzi wanaoenda vyuoni wapimwe matumizi ya dawa za kulevya’ | Millardayo

Sina Beef Na Mange Kimambi Ananipenda Na Ananikubali : Wolper – Jicho La Uswazi | Mcinika Wa Lamar

KESI YA KUPINGA KUONDOLEWA CHANEL ZA NDANI KWENYE VISIMBUZI KUTAJWA OCTOBA 18 | Darmpya

MAMILIONI YA MFUKO WA JIMBO NYAMAGANA YAMWAGWA SOKO LA MLANGO MMOJA. | Darmpya

Popular This Month

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA BILL GATES NA KAIMU BALOZI WA MAREKANI NCHINI | MICHUZI BLOG

HISTORIA YA WANGONI NA LILIPOTOKA JINA LA SONGEA | noreply@blogger.com (Lewis Mbonde)

Dubai yazindua jengo refu zaidi duniani lenye ghorofa 75 | Darmpya

Birdman wa CashMoney anakuja Tanzania | Millardayo

Popular All Time

MPOGOLO AWATAKA VIONGOZI MKOANI DODOMA KUSHUKA CHINI KUIMARISHA MASHINA…WAKULIMA WA ZABIBU WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI. | Darmpya

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

MSUVA AWA MTAMU APIGA MBILI PEKE YAKE, DIFAA EL JADIDA | Darmpya

MABONDIA WAWILI WA TANZANIA WACHEZEA KICHAPO USIKU MMOJA | Darmpya

“SIJAONA SIMBA YA KUIFUNGA AZAM KESHO” – NGAONA | Darmpya

MAFUNDI UMEME WATAKIWA KUWA NA LESENI YA EWURA KUPUNGUZA ‘VISHOKA’ NJOMBE | Darmpya

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

BABA NA MWANAE NA SHEMEJI MTU WAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA | Darmpya