Trump amekataa kuahidi kukubali matokeo ya uchaguzi akishindwa


Trump na ClintonImage copyright

Mgombea wa urais kupitia tiketi ya chama cha Democrat Donald Trump amesema kuwa atakubali matokeo ya uchaguzi wa urais nchini Marekani ''iwapo atashinda'' .

Amesema kuwa atakubali matokeo ya moja kwa moja yasio na udanganyifu wowote akiongezea kuwa ana haki ya kupinga matokjeo hayo iwapo hayatakuwa na utata.

Alionekana katika mkutano mjini Delaware jimbo la Ohio ,akizungumza kwa mara ya kwanza baada ya mjadala wa tatu wa urais dhidi ya mpinzani wake wa chama cha Democrat Hillary Clinton.

Bwana Trump amekuwa akikosolewa kwa kusema kuwa hatakubali matokeo ya uchaguzi huo.

Donald Trump alikataa kuahidi kukubali matokeo ya uchaguzi iwapo atashindwa, katika mjadala wa mwisho wa urais dhidi ya Hillary Clinton.

"Nitakuambia wakati huo" alimwambia muendesha mjadala Chris Wallace. Kwa siku kadhaa amedai kuwa kuna 'udanganyifu' katika uchaguzi huo.

Mjadala huo wa televisheni Las Vegas uliendeleza uhasama katika kampeni huku Trump akimuita Bo Clinton "mwanamke muovu".

Kura za kutafuta maoni zinaonyesha Trump poteza umaarufu katika majimbo makuu baada ya kukabiliwa na tuhuma za unyanyasaji wa kingono.

Mjadala huo wa mwisho wa umefanyika wiki tatu kabla ya siku ya uchaguzi Novemba 8.

Wagombea hao walikataa kusalimiana kwa mikono kabla na baada ya majibizano hayo ya kisiasa, hatua iliyofungua kile ambacho baadaye kiligeuka kuwa mjadala wa kelele na kukatizana kauli.

Trump alitoa ahadi kwa wanachama wa Republican kuwateua majaji wa mahakama ya juu zaidi wanaoegemea 'mrengo wa kihafidhina' watakaogeuza sheria kuu inayohalalisha uavyaji mimba Marekani na kulinda haki za kumiliki bunduki.

ClintonImage copyrightAP

Alisisitiza ahadi yake ya kuwarudisha nyumbani wahamiaji ambao hawakusajiliwa na kudhibiti mipaka ya Marekani.

Wakati huo huo, Bi Clinton ametangaza wazi kuwa atawatetea wapenzi wa jinsia moja, atalinda haki za kuavya mimba, atalenga kuinusha watu wa kipato cha wastani na kushinikiza kulipwa sawa kwa wanawake.

"Serikali haina shughuli yoyote katika maamuzi wanayofanya wanawake," alisema.

Katika mojawapo ya nyakati zilizokuwa na mvuto, Trump alikataa mara mbili kusema iwapo atakubali matokeo ya uchaguzi, hatua iliyobadili utamaduni wa muda mrefu wa wagombea wanaoshindwa kukubali matokeo baadaya kura kuhesabiwa.

"Hilo ni jambo la kuogofya," Clinton akajibu kwa ukali.

"Anaponda na kudharau demokrasia yetu. Na mimi kivyangu, nimeshangazwa kuwa mtu ambaye ni mgombea mteule wa mojawapo wa vyama viwili vikuu anaweza kuchukua msimamo wa aina hiyo."

Trump alisindikizwa na familia yake baada ya mjadala kumalizikaImage copyright
Image captionTrump alisindikizwa na familia yake baada ya mjadala kumalizika

Majibu ya Trump yamezusha shutuma kali kutoka kwa seneta wa Republican Lindsey Graham, aliyesema mgombea huyo "hawajibi ipasavyo kwa chama chake na taifa kwa kuendelea kuashiria kuwa anafanyiwa udanganyifu katika uchaguzi ujao," kwa mujibu wa taarifa.

Kauli nyingine kuu katika mjadala katika chuo kikuu cha Nevada ni :

  • Bi Clinton anasema Putin anataka Trump achaguliwe kwasababu anataka kinyago awe rais wa Marekani.
  • "Tuna watu wabaya na tuta watoa," amesema Trump, aliposhinikiza ahadi yake ya kujenga ukuta mpakani.
  • Bi Clinton amesema ataidhinisha mpango mkubwa wa ajira kuwahi kushuhudiwa tangu vita vya pili vya dunia.
  • Trump ameashiria bi Clinto na rais Barack Obama walipanga ghasia katika mkutano wake wa kisiasa Chicago mapema mwaka huu.

Comments

Popular This Week

IGP SIRRO:NCHI YETU IKO SALAMA, NA TUNAO UWEZO WA KUFANYA UCHUNGUZI | Darmpya

MBUNGE SINGIDA MAGHARIBI ELIBARIKI KINGU (CCM) AWEKA HISTORIA | Darmpya

TAWLA YATOA MAFUNZO YA JINSI YA KUSHUGHULIKIA WATOTO WALIO KATIKA UKINZANI NA SHERIA | VIJIMAMBO

Wasanii watakaokiwasha Tigo Fiesta jijini Mwanza watembelea Duka la Tigo leo. | Mrisho’s Photography

“Ukipata mshtuko wa moyo, usipopata huduma ndani ya dk 90 ni kifo” – JKCI | Millardayo

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

MSUVA AWA MTAMU APIGA MBILI PEKE YAKE, DIFAA EL JADIDA | Darmpya

Popular This Month

IGP SIRRO:NCHI YETU IKO SALAMA, NA TUNAO UWEZO WA KUFANYA UCHUNGUZI | Darmpya

TAWLA YATOA MAFUNZO YA JINSI YA KUSHUGHULIKIA WATOTO WALIO KATIKA UKINZANI NA SHERIA | VIJIMAMBO

MBUNGE SINGIDA MAGHARIBI ELIBARIKI KINGU (CCM) AWEKA HISTORIA | Darmpya

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

Wasanii watakaokiwasha Tigo Fiesta jijini Mwanza watembelea Duka la Tigo leo. | Mrisho’s Photography

“Ukipata mshtuko wa moyo, usipopata huduma ndani ya dk 90 ni kifo” – JKCI | Millardayo

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

Majeshi ya Iraq yapiga hatua kuishambulia IS

Popular All Time

MPOGOLO AWATAKA VIONGOZI MKOANI DODOMA KUSHUKA CHINI KUIMARISHA MASHINA…WAKULIMA WA ZABIBU WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI. | Darmpya

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

MSUVA AWA MTAMU APIGA MBILI PEKE YAKE, DIFAA EL JADIDA | Darmpya

MABONDIA WAWILI WA TANZANIA WACHEZEA KICHAPO USIKU MMOJA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

“SIJAONA SIMBA YA KUIFUNGA AZAM KESHO” – NGAONA | Darmpya

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

BABA NA MWANAE NA SHEMEJI MTU WAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA | Darmpya

MAFUNDI UMEME WATAKIWA KUWA NA LESENI YA EWURA KUPUNGUZA ‘VISHOKA’ NJOMBE | Darmpya