Asema alilazimishwa kukiri kumuua Kim Jong nam na Malaysia
Mtu mmoja
anayeshukiwa kuhusika na mauji ya ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea
Kaskazini Kim Jong Un, amesema kuwa yeye ni mhanga wa hujuma za utawala
wa Malaysia dhidi ya Korea Kaskazini.
Akizungumza mjini Beijing
baada ya kuwasili kutoka Malaysia, Ri Jong Chol, amelaumu polisi wa
Malaysia, kwa kutishia familia yake, iwapo hatakiri kuhusika kwake na
mauaji ya Kim Jong Nam. Hapo jana Ijumaa maafisa nchini Malaysia walisema, wana ushahidi wa kutosha, kumfungulia mashtaka Bw. Ri, na kwamba atarejeshwa kwao kwa kosa la kukiuka sheria ya uhamiaji ya nchi hiyo.
Comments