JOHN HECHE:WATU HAWAKO SALAMA NCHI HII, NI BAADA YA MDOGO WAKE KUUAWA NA POLISI | Darmpya

Mbunge wa Tarime Vijijini kupitia (CHADEMA), mheshimiwa John Heche, amesema mdogo wake anayejulikana kwa majina ya Suguta Chacha, ameuuawa kwa kuchomwa kisu na polisi wa kituo cha Sirari usiku wa kuamka leo.

Mbunge huyo amedhibitisha kuuawa kwa ndugu yake huyo katika ujumbe wake kwenye ukarasa wake wa mtandao wa Twitter kuwa leo Aprili 27 2018 na kusema kuwa Suguta alichomwa kisu na polisi waliomkamata baada ya kumkuta baa akinywa pombe. Inadaiwa polisi wametekeleza tukio hilo huku akiwa na pingu mkononi.

“Watu hawako salama tena mikononi mwa polisi. Mdogo wangu Suguta amekamatwa na polisi jana usiku na ameuwawa na polisi kwa kuchomwa kisu. Najisikia maumivu mno, hii sio nchi ambayo tunaitaka. Najiuliza maswali mengi ni kwa vipi mtu amefungwa pingu anachomwa kisu tena na polisi.” Aliandika hivyo Mhe. Heche.

Aidha, Kamanda wa polisi mkoa Mara, RPC Mwibambe amethibitisha kutokea tukio hilo na wananchi wakazi wa Sirari wamezingira kituo hicho cha polisi baada kusikia kijana huyo ambaye inasemekana ana umri wa miaka 29 mkazi wa Sirari wilayani Tarime, kupoteza maisha akiwa mikononi mwa polisi.



from Dar Mpya Online TV

Comments

Popular This Week

DIWANI WA CCM APOTEZA MAISHA KWA AJALI ASUBUHI YA LEO. | Darmpya

IGP SIRRO:NCHI YETU IKO SALAMA, NA TUNAO UWEZO WA KUFANYA UCHUNGUZI | Darmpya

MAHAKAMA NCHINI ZAMBIA YAAGIZA MWANAMUZIKI KOFII OLOMIDE KUKAMATWA. | Darmpya

MBUNGE KUBENEA AMUUMBUA RC MAKONDA , | Darmpya

Popular This Month

AUDIO | DJ Mwanga

DIWANI WA CCM APOTEZA MAISHA KWA AJALI ASUBUHI YA LEO. | Darmpya

IGP SIRRO:NCHI YETU IKO SALAMA, NA TUNAO UWEZO WA KUFANYA UCHUNGUZI | Darmpya

MAHAKAMA NCHINI ZAMBIA YAAGIZA MWANAMUZIKI KOFII OLOMIDE KUKAMATWA. | Darmpya

RAIS NA MWENYEKITI WA CCM DKT MAGUFULI AENDESHA KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHAMA JIJINI DAR ES SALAAM LEO | noreply@blogger.com (Muhidin Sufiani)

VIDEO | DJ Mwanga

House Victimz – Victimized Vol.1 Album | AutoMedia Tanzania

Popular All Time

MPOGOLO AWATAKA VIONGOZI MKOANI DODOMA KUSHUKA CHINI KUIMARISHA MASHINA…WAKULIMA WA ZABIBU WAMPONGEZA RAIS MAGUFULI. | Darmpya

KOROSHO TANI 68 ZAREJESHWA KWA WAKULIMA KWA KUKOSA UBORA | Darmpya

VIJIJI 20 MKOANI NJOMBE KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME UNAOFADHILIWA NA UJERUMANI | Darmpya

MSUVA AWA MTAMU APIGA MBILI PEKE YAKE, DIFAA EL JADIDA | Darmpya

MABONDIA WAWILI WA TANZANIA WACHEZEA KICHAPO USIKU MMOJA | Darmpya

“SIJAONA SIMBA YA KUIFUNGA AZAM KESHO” – NGAONA | Darmpya

MAFUNDI UMEME WATAKIWA KUWA NA LESENI YA EWURA KUPUNGUZA ‘VISHOKA’ NJOMBE | Darmpya

NYAMAGANA YAPATA KM 45 ZA MRADI WA UMEME VIJIJINI (REA) | Darmpya

BABA NA MWANAE NA SHEMEJI MTU WAHUKUMIWA MIAKA 30 JELA | Darmpya