Wasiwasi waendelea Duniani kuhusu simu hatari ya Galaxy note 7
Samsung kuwatumia wateja wake walioko Marekani makasha yanayoweza kustahimili moto, kuweka Note 7 wanazorejesha Kampuni ya vifaa vya eletroniki ya Samsung imetangaza kuwatumia wateja wake walioko Marekani makasha yanayoweza kustahimili moto, kama tahadhari dhidi ya uwezekano wa kutokea moto au kulipuka kwa simu zake aiana ya Galaxy Note 7 walizorejesha kwa wauzaji simu hizo nchini humo. Makasha hayo hasa yanatolewa kwa wateja walionunua simu hizo katika tovuti yake ya Samsung.com. Walio na simu hiyo aina ya Galazy Note 7 pia wameshauriwa kutembelea tovuti ya Samsung kufahamu maelekezo ya kuzirejesha. Kampuni hiyo ya Samsung imetangaza kusitisha utengenezaji wa simu hiyo ya Galazy note 7 miezi miwili baada ya kuizindua upya, baada ya kurekebishwa mara ya pili, kufuatia ripoti kadhaa za simu hiyo kushika moto.Samsung sasa italazimika kupokea zaidi ya Galazy Note 7 million 1.5 ilizokuwa tayari imeuza au kutoa kama simu mbadala. Nyingi ya simu hizo ziliuzwa Marekani na Korea Kusini. Hata i...