Clinton na Trump wataniana kwenye dhifa New York
Image copyright AP Image caption Hafla hiyo huchangisha mamilioni ya dola kusaidia watoto wasio na uwezo na watu maskini Wagombea wakuu wa urais nchini Marekani Hillary Clinton na Donald Trump walirushiana vijembe kwa utani katika dhifa ya jioni iliyoandaliwa kuchangisha pesa za hisani. Walishiriki kwenye dhifa hiyo siku moja baada ya kushambuliana vikali kwenye mdahalo wa mwisho wa runinga. Bi Clinton alicheka sana Bw Trump alipomtania kuhusu hotuba za kulipwa na pia uchunguzi wa FBI kuhusu tuhuma kwamba alitumia barua pepe ya kibinafsi kwa shughuli rasmi. Lakini Bw Trump alizomewa alipofanya mzaha kwamba mpinzani huyo wake huwachukia Wakatoliki. Dhifa hiyo ya Wakfu wa Ukumbusho wa Alfred E Smith mjini New York hufanyika kila baada ya miaka minne na kuwashirikisha wagombea urais. Kuna desturi kwamba wagombea husimama na kutaniana, lakini mwana huu imeandaliwa wakati kumekuwa na uhasama mkubwa sana kwenye kampeni. Trump v Clinton: Nani anaongoza? Trump: Kura zinaibiwa vituoni Marekani ...